Saturday, 16 November 2013

ZIJUE FAIDA ZA ASALI

                                                         

ZIJUE FAIDA ZA ASALI


Asali imekuwepo toka enzi za mababu zetu lakini watu bado hawajaelewa umuhimu wa kutumia asali, hasa Asali Halisi (Asali Mbichi). Watu wengi wamekuwa wakipata shida za kiafya kutokana na matumizi mabaya ya vyakula, ikiwemo uvIvu wa kufanya mazoezi. Asali ni mkombozi wa matatizo mengi ya kiafya yanayomsumbua mwanadamu;
                                                                           

Wataalamu wa afya waliofanya utafiti kuhusu asali na uwezo wa kupunguza unene walibaini kwamba, muda wa saa nne za mwanzo za usingizi, asali itayeyusha mafuta mengi mwilini sawa na kufanya mazoezi makali. Tumia asali vijiko 2 vya chai kila unapokwenda kulala, ni vizuri zaidi tiba hii ikaambatana na kufanya mazoezi kiasi. Umuhimu wa asali kwenye tatizo la unene ni uwezo wake wa kuyeyusha mafuta mwilini kwa haraka ukiwa umelala na wakati huo huo kuupa mwili nguvu. Hii ni kwa tatizo la unene, lakini unaweza kutumia asali kwa matumizi mengine.
                                         
                                      


ASALI MBICHI(ASALI HALISI), ZAO LA TANZANIA

Eben-Ezery Mende kwenye Jambo Leo, Jumamosi ya tarehe 11 Mwezi wa Tano, 2013 aliweza kueleza mambo mengi kuhusiana na umuhimu wa Asali na hasa Asali Mbichi;

Unaweza kutumia asali na mdalasini kwa kuchanganya, umoja huo umebainika kusaidia kupunguza uzito. Mchanganyiko huo unatakiwa uwe wa asali na unga wa mdalasini. Baada ya kuchanganya vizuri asali na mdalasini Utapata kinywaji kama ilivyo vinywaji vingine ambapo utatakiwa kuchanganya asali, mdalasini na maji ya moto.

Ukivichanganya vitu hivyo ni tayari kwa matumizi na hapo unapaswa kunywa mara mbili kwa siku. Chukua nusu kijiko cha unga wa mdalasini (kijiko kidogo cha chai) kijiko kimoja cha asali  na kikombe kimoja cha maji yaliyochemka.

Hatua ya kwanza ni kuchanganya maji moto na unga wa mdalasini, koroga hadi uchanganyike vizuri kisha funika na uache muda wa nusu saa ili maji yapoe. Baada ya maji kupoa, weka asali kijiko kimoja kisha koroga tena hadi mchanganyiko uwe kama kinywaji.

Asilimia 98 ya watu duniani wanafahamu vema kwamba mojawapo ya silaha ya ajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee ni kwa kutumia asali.

Utafiti mpya umeonesha uwezo wa asali huongezeka maradufu ikichanganywa na mdalasini katika kutatua tatizo la uzito na kumfanya mtu kuwa na uwezo mkubwa wa fikra na kumbukumbu.

Uchunguzi ufanywao na Jarida la World News uliohusu tiba, wataalamu wa dawa zitokanazo na mimea na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kuna umuhimu wa asali na mdalasini kwakuwa mchanganyiko huo ni dawa ya kusisimua iletayo afya bora.

Pia asali inatatua tatizo la ugonjwa wa viungo na uvimbe ambapo wataalamu wa lishe wanapendekeza kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja cha chai chenye mdalasini na kuchua sehemu zilizohathirika.

Tiba hiyo inaanza kuonesha matunda yake kwa kupata nafuu dakika moja baada ya kutumiwa.

Kama hiyo hutaimudu unashauriwa kutengeneza chai kikombe kimoja chenye maji ya moto, weka vijiko vya chakula viwili vya asali kwa kijiko cha chai cha mdalasini kisha unywe asubuhi na jioni ili kuondoa maumivu.

Utafiti uliofanyika hivi karibuni na Chuo Kikuu Copenhagen, madaktari waliwapa wagonjwa 200, syrup mchanganyiko wa kijiko kimoja cha chai cha asali na kimoja cha mdalasini kila asubuhi kabla ya kifungua kinywa walipata ahueni.

Hata hivyo imebainika kwamba asilimia 73 ya walioripotiwa kupata ahueni kubwa ya maumivu na ongezeko katika kufanya shughuli kama kujongea na kutembea vema.

Mbali ya faida nilizozieleza awali pia katika urembo asali hutumika na hapa unaweza kuitumia kwa kulinda kukatika kwa nywele.

Asali ikishachanganywa na mdalasini na mafuta vuguvugu ya olive, hutoa kichocheo cha kuotesha nywele kinachotumika katika dawa ya Dork. Mchanganyiko huo vuguvugu unapakwa kwa kusugua kichwani na kuachwa kwa dakika 15.

Tiba nyingine inayotokana na asali ni ukungu wa miguuni ambapo unatakiwa kuchanganya kijiko kikubwa cha mezani cha asali, vijiko viwili vya mdalasini. Paka sehemu zilizoathirika usiku kwa muda wa nusu saa, kisha safisha kwa sabuni na maji. Tatizo litakwisha baada ya wiki moja.

Hili nalo ni kubwa ambalo asali hutumika kulitibu ambalo ni maambukizi kwenye kibofu cha mkojo.

Chukua glasi ya maji vuguvugu yaliyochanganywa na vijiko viwili vya chai vya mdalasini na kijiko kimoja cha chai cha asali huondoa bakteria kwenye kibofu. Pia unaweza ukatumia juisi ya cranberry badala ya maji ikiwa ambukizo la kibofu litakuwa sugu.

Mtu mwenye maumivu ya jino anaweza kuchanganya sehemu tano za asali na sehemu moja ya mdalasini na tumia kwa maumivu ya jino kwa kudondoshea kwenye jino au meno yaliyoathirika hadi maumivu yatakapotoweka.

Saladi ya kupaka vidonda iliyochanganywa na asali na mdalasini kwenye chai ya raspberry nyekundu ni dawa nzuri ya kuondoa maumivu makali ya vidonda vitokanavyo na kulala muda mrefu.

Hizo ni baadhi tu ya faida za asali lakini kila tatizo katika mwili wa binadamu lina nafasi ya kutumia asali kwa kuchanganya  chakula au kimiminika kingine na mgonjwa akapona kabisa ugonjwa unaomsumbua.

Mwandishi wa safu hii si daktari wala muuguzi bali yanayoandikwa yanatokana na tafiti, vyanzo vya habari kwa ushirikianao na wataalamu wa afya ya binadamu.



Ukihitaji Asali Mbichi (Asali Halisi), waweza kutupata,



You Can Find Us,

Mayfair Plaza-Central Building,

Mwai Kibaki Road,

Dar es Salaam – Tanzania.

Cell : +255 767 510 564 / 688 510 564 

Email : recafotz@gmail.com. 

 Blog : PureNaturalHoney-AsaliHalisi.blogspot.com        
  

1 comment:

  1. Nyuki ni Tabibu wa kwanza hapa duniani, maana Mungu alimfanya hivyo ili wanadamu tufaidi matunda yake. Madaktari wanaweza kutengeneza dawa, vyakula na mambo mengi, lakini sio kama afanyavyo mdudu huyu mwenye uwenzo mkubwa wa kitabibu. Anatengeneza asali ambayo inaweza tumika kama: chakula, kinywaji, dawa, kipodozi au kiungo. Magonjwa karibia yote huweza kutibika kwa mazao ya mdudu huyu nyuki. Jamani nyuki ni kiumbe aliye barikiwa na Mungu. Tumia Asali Mbichi kwa afya ya familia yako.

    ReplyDelete